
Mwenyekiti wa chama cha madereva wa malori na mabasi ya Masafa Marefu Tanzania (TLDTA) Hassan Dede amewahimiza waandishi wa habari kufanya kazi kwa uzalendo kwa ajili ya nchi yao.
Dede ameyasema hayo wakati wa iftar mahususi aliyoandaa kwa ajili ya waandishi wa habari Jijini Mwanza
Amesema waandishi wa habari wana mchango mkubwa katika maendeleo ya katika nchi hivyo ameona ni vyema kujumuika nao pamoja kama ishara ya umoja mshikamano na upendo katika mwezi mtukufu wa Ramadhan na kwaresma.
Akizungumza kwa niaba ya Waandishi wa habari mkoani mwanza George Binagi amemshukuru Dede kwa kuthamini mchango wao kwani futari hiyo imeimarisha umoja na mshikamano kwa wanahabari na wadau mbalimbali jijini Mwanza.







