Na Mwandishi wetu.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akiweka jiwe la msingi, kuashiria kuzindua rasmi ujenzi wa Ofisi za Makao Makuu ya CCM, katika hafla iliyofanyika eneo la Tambuka reli, jijini Dodoma, litakapojengwa jengo hilo.
Uzinduzi huo uliohudhuriwa na maelfu ya wananchi mbalimbali, wakiongozwa na viongozi na wanachama wa CCM, umefanyika leo Jumatano, tarehe 28 Mei 2025.
#NTTUpdates