×
New Times Tanzania New Times Tanzania is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services.
New Times Tanzania

MATHYS TEL AJIUNGA NA SPURS KWA MKOPO

Na Mwandishi wetu.

Klabu ya Tottenham Hotspur ya Uingereza imefanikiwa kumpata kwa mkopo winga wa kushoto Mathys Henri Tel (19) raia wa Ufaransa akitokea Bayern Munich ya Ujerumani.

Tel ambaye hajawa na wakati mzuri kwenye kikosi Cha Bayern Munich chini ya kocha Vicent Kompany amejiunga na Spurs ili kupata nafasi zaidi ya kucheza na kuendeleza kipaji chake Uingereza.

Tel amecheza michezo 14 akitoa assist moja pekee kwenye michuano yote ambayo klabu ya Bayern Munich imeshiriki msimu huu.

#NTTupdates