Na Mwandishi wetu.
Washika mitutu wa ligi kuu ya EPL nchini Uingereza, Arsenal wameweka wazi kuwa mlinzi wao wa kushoto kinda Myles Anthony Lewis-Skelly (18) raia wa Uingereza ataendelea kusalia klabuni hapo kwa sababu miongoni mwa wachezaji ambao wanaowahitaji kwa muda mrefu ili kufanikisha project yao.
Arsenal umeandaa pendekezo jipya la mkataba ili kumfanya mlinzi huyo kuendelee kusalia klabuni hapo kutokana na kiwango kizuri alichokionyesha chini ya kocha Mikel Arteta toka apandishwe kutoka timu ya vijana.
Myles Skelly ambaye pia anauwezo wa kucheza nafasi ya Kiungo msimu huu ameitumikia Arsenal kwenye michezo 16 akipewa Kadi 2 za njano kwenye michuano yote ambayo Arsenal imeshiriki.
#NTTupdates