Na Mwandishi wetu.
Klabu ya Kaizer Chiefs maarufu kama Amakhosi imeachana na mlinzi wao Edmilson Gabriel Dove ( 30) Raia wa Mozambique baada ya kimaliza mkataba wake.
Dove ambaye alijiunga na Kaizer Chiefs mwaka 2022 amecheza michezo zaidi ya 56 na akitajwa kama miongoni mwa mabeki Bora waliowahi kucheza kwenye klabu hiyo.
Edmilson Dove kupitia mitandao yake ya kijamii amewashukuru viongozi wa klabu hiyo na mashabiki kwa upendo na sapoti yao kipindi chote akiwa Kaizer Chiefs.
#NTTupdates