Na Mwandishi wetu.
Chifu wa Kabila Wahehe Adam Abdul Adam Sapi Mkwawa wa pili akimkaribisha Mgombea wa Nafasi ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Dkt. Samia Suluhu Hassan mara baada ya kuwasili Kalenga mkoani Iringa katika muendelezo wa Kampeni za Uchaguzi Mkuu kwa Chama hicho mkoani humo tarehe 06 Septemba, 2025.
Chifu huyo wa Kabila la Wahehe alisimama katika eneo la Kichuguu cha Kidundaa ambalo Chifu wa Kabila hilo Mtwa Mkwawa alikuwa akilitumia wakati akizungumza na watu wake wa Kalenga.
#NTTupdates