Na Mwandishi wetu.
Mshambuliaji wa Kimataifa wa Guinea na klabu ya Borrusia Dortmund ya Ujerumani Serhou Yalady Guirassy (29) amekabidhiwa rasmi kiatu chake Cha Dhahabu cha ufungaji Bora wa ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA).
Guirassy ambae alimizia msimu uliopita akiwa na magoli 13 kwenye ligi ya Mabingwa Ulaya (UEFA) huku akifunga magoli 21 kwenye ligi kuu Ujerumani (Bundesliga) nyuma ya kinara Harry Kane aliyemaliza akiwa na Magoli 26.
Majarida mbalimbali ya Michezo Ulaya yamemtaja Guirassy kama mshambuliaji hatari kwa sasa barani Ulaya.
#NTTupdates