×
New Times Tanzania New Times Tanzania is a multi-media organization with investments in media platforms spanning newspaper print operations, television, radio broadcasting, digital and online services.
New Times Tanzania

MWENGE WA UHURU WAZINDUA OFISI YA KATA WILAYA YA MWANGA

Na Mwandishi wetu.

Mwenge  wa Uhuru mwaka 2025,  umezindua Ofisi ya kijiji cha Ngulu kilichopo kata ya Kwakoa Wilaya  ya Mwanga Mkoani Kilimanjaro, ikiwa ni hatua za Serikali za kuboresha mazingira ya watumishi katika utendaji kazi.

Akizungumza  wakati wa uzinduzi huo, Julai 1, 2025 kiongozi wa mbio za Mwenge, Ismail Ali Ussi  amesema, Serikali imedhamiria kuboresha mazingira ya watumishi ili wananchi waweze kupata  huduma iliyo bora kwa  haraka na kwa wakati husika.

Aidha, amewataka watumishi watakaofanya kazi katika eneo hilo kufanya kazi kwa uwaminifu na kwa haraka ili kuwasaidia wananchi katika utatuzi wa changamoto mbalimbali zitakazokuwa zikiwasilishwa Ofisini hapo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Mwaga Bi. Rukia amesema kuwa kwasasa wananchi wa eneo hilo wataweza kutatuliwa matatizo yao kwa haraka na kwa wakati kutokana na kukamilika kwa ofisi hiyo kwani hapo awali kulikuwa na ofisi isiyokidhi mahitaji muhimu yanayotakiwa katika utendaji wa kazi.

Akisoma taarifa ya mradi huo, Bi. Angela Kilawe  amesema hadi kukamilika kwa jengo la Ofisi hiyo jumla ya kiasi cha shillingi million 56 zimetumika.

#NTTupdates.