Na Mwandishi wetu.
Mchezo wa mapema hatua ya nusu fainali ya Ngao ya Jamii unapigwa leo kwenye uwanja wa KMC Complex uliopo Mwenge Dar es Salaam majira ya saa 7:00 mchana ukiwakutanisha JKT Queens dhidi ya Ceasiaa Queens ya mkoani Iringa.
Vilabu hivyo, vimetambiana kila upande ukiahidi kupata ushindi kwenye mchezo huo na kutinga fainali.
Mshindi wa mchezo huo atakutana na mshindi kati ya Simba Queens au Yanga Princess ambao wao watashuka dimbani saa 10:00 Jioni kwenye uwanja huo huo.
#NTTUpdates