
Bodi ya ligi kuu Tanzania Bara (TPLB) imetangaza rasmi kufanya mabadiliko ya uwanja kuelekea mchezo namba 169 kati ya Mnyama Simba SC dhidi ya Wananchi Young Africans SC ambapo sasa mchezo huo utapigwa katika dimba la Jenerali Isamuhyo uliopo Mbweni tarehe 3 May 2026 badala ya Benjamin Mkapa.
Sababu za kuhamishwa mchezo huo ni kuwepo kwa ukarabati unaoendelea kwenye dimba la Benjamini Mkapa kuelekea michuano ya AFCON 2027.